This is the html version of the file http://www.uoguelph.ca/rocks/Fosiforasi%20Katika%20Kilimo%20-%20Kiswahili.pdf.
Google automatically generates html versions of documents as we crawl the web.
SOIL FERTILITY
Page 1
Karibu!
Maelezo haya yametayarishwa kwa ajili ya maafisa ugani wanaofanyakazi
na mashirika yasiyo ya kiserikali, mashirika ya kijamii, taasisi za utafiti au
idara za ugani kitaifa zinazoshirikiana na mradi wa "Rocks for Crops"
unaofadhiliwa na Jumuia ya Madola. Hata hivyo tunategemea maelezo
haya yatatumika na watu wengine wanaofanyakazi na vikundi vya wakulima.
Itakuwa ni vema kama rasilimali hii itatumika na kusambazwa kwa wadao wengi
zaidi.
Ujumbe huu unaelezea fosiforasi, mojawapo ya virutubisho muhimu vya mimea.
Mara nyingi fosforasi huisha haraka katika udongo. Kutambua tatizo hili ni hauta
muhimu itakayosaidia kutatua tatizo. Ujumbe huu unalenga kusaidia maafisa
ugani kuwa na maelezo yanayohitajika na vikundi vya wakulima ili kukuza
uelewa kuhusu umuhimu wa kirutubisho cha fosiforasi katika rutuba ya udongo.
Kwa kutumia njia shirikishi, vikundi vya wakulima vitaweza kutambua dalili za
upungufu wa fisiforasi katika udongo wakielekezwa na maafisa ugani au bwana
shamba.
Maneno muhimu na maana zake yameorodheshwa katika ujumbe huu pamoja
na kumbukumbu ya vitabu vilivyotumika kutengeneza maelezo haya. Kuna picha
na michoro ambayo imeingizwa katika maelezo haya kwa ajili ya maafisa ugani
kutumia kujadiliana na vikundi vya wakulima. Vielelezo hivi vinaweza kutumika ili
kufanya somo lieleweke kwa urahisi.
Tunategemea ujumbe huu utakuwa zana yenye manufaa.
Shukrani
Tunawashukuru sana wote ambao wamehusika katika matayarisho ya ujumbe
huu. Shukrani nyingi kwa walioleta picha pamoja na maelezo ambayo
yameongeza thamani ya ujumbe huu. Mchango uliotokana na washiriki wenzetu
utafanya ujumbe huu ufae na kutumiwa na wale wote wanaofanyakazi kwa moyo
katika kuboresha maisha ya wakulima wadogo wadogo katika nchi zao.
1

Page 2
Fosiforasi katika kilimo
Udongo ni muhimu kwa maisha endelevu ya mwanadamu, lakini tayari sehemu
kubwa ya kusini mwa jangwa la Sahara barani Afrika lina tatizo la rutuba ndogo
ya udongo. Kwa nini kuna tatizo hili? Wakulima wafanyeje kuboresha rutuba ya
udongo na hatimaye waweze kupata chakula cha kutosha kwa ajili ya familia
zao?
Kuna mambo mengi yanayokwamisha wakulima wadogo wadogo katika Afrika
kuweza kuzalisha mazao kwa wingi au kiwango kinachotakiwa. Baadhi yake ni:
Hali ya hewa (mvua ndogo, mvua nyingi, jua kali kubadilika kwa hali ya hewa
n.k)
Wadudu na magonjwa.
Magugu yanayo9sumbua sana kama viduha.
Umaskini.
Ukosefu wa nguvu kazi.
Jambo lingine kubwa lililotambuliwa ambalo linapunguza sana rutuba ya udongo
katika nchi zilizoko kusini mwa jangwa la Sahara ni upungufu wa virutubisho
katika udongo. Nitrojeni ni tatizo kubwa na inahitajika sana ili kuboresha
uzalishaji wa mazao ikifuatiwa na kirutubisho cha aina ya fosiforasi.
2
Utangulizi
Mimea ya mahindi iliyopandwa kama sehemu ya mafunzo katika shule ya migodi, chuo kikuu cha Zimbabwe.
Mahindi haya yote yalipandwa siku moja lakini kila ndoo imetiwa kiwango tofauti cha mbolea ya fosiforasi
kama ilivyooandikwa katika kila ndoo. Picha hii inaonyesha jinsi mbolea hii inavyoweza kuboresha ukuaji na
uzalishaji wa mazao. Picha hii imepigwa na Victor Shitumbanuma.

Page 3
Pamoja na kwamba wakulima wadogo wadogo wanahangaika kulima mazao ya
kutosha kwa ajili ya kulisha familia zao, udongo ulioko kwenye mashamba yao
una kiasi kidogo cha kirutubisho cha fosiforasi na hawana uwezo wa kununua
mbolea za viwandani kutatua tatizo hili.
Kwa hiyo ni namna gani maafisa ugani watashirikiana na wakulima hawa na
kuwafundish namana ya kutambua kama mazao yao yanaathirika na kiasi kidogo
cha fosiforasi katika udongo? Ni namna gani tunaweza kuwasaidia wakulima
katika kuchagua njia zitakazofaa kurutubisha udongo?
Picha hii imechorwa na Elijah Njoroge
Wakulima wengi wadogo wadogo wanashindwa kutatua tatizo hili la upungufu wa
fosiforasi katika mashamba yao kwa sababu wana uwezo mdogo kupata
pembejeo, hizi zote za aina mbili za asilia na viwandani. Kama afisa ugani,
3
Katika kurasa zifuatazo, utajifunza kuhusu asili ya fosiforasi (pia inajulikana kama P)
katika udongo, umuhimu wake katika ukuaji wa mmea, na namna udongo unavyokuja
kuwa na upungufu wa fosiforusi. Mapendekezo ya namna ya kufanyakazi na
wakulima ili kuweza kutambua dalili zinazoonyesha upungufu wa fosiforusi katika
udongo pia zimelezwa mwiho kuna maelezo kwa ufupi kuhusu mbinu mbalimbali za
namna ya kutatua tatizo hili.

Page 4
unaweza kushirikiana na wakulima kuweza kutambua maeneo ambayo
yanamatatizo sana ya upungufu wa virutubisho vya mimea.
Foriforasi ni moja ya virutubisho muhimu (ikiwa ni pamoja na Naitrogeni na
Potasiumu) sana katika ukuaji wa mazao. Kirutubisho hiki kiwingi asili yake ni
kutoka katika miamba kama vile miamba ya fosiforasi ("Phosphate Rocks") kuna
aina mbili za fosiforasi katika udongo yaani fosiforusi iliyotoka moja kwa moja
katika miama na ile inayotokana na uozaji wa viumbe hai? Mboji samaji n.k.
Aina zote hizi mbili ni muhimu kwa ukuaji wa mimea.
Udongo unaweza ukawa na fosiforasi nyingi lakini inayohitajika ni ile ambayo
inaweza kuyeyuka na kuchukuliwa na mimea. Mambo yafuatayo ndio yanaweza
kufanya au kuzuia fosiforasi iliyoko katika udongo iwe katika hali ya kuchukuliwa
na mmea.
➢ Tindikali (pH) ya udongo
➢ Madini ya chokaa chuma na aluminiamu katika udongo.
➢ Kiasi cha mboji iliyooza katika udongo
➢ Makazi ya viumbe hai katika udongo.
Kwa mfano katika udongo wenye chachu tindikali kiwango cha fosiforasi inakuwa
imeshikiliwa na madini ya chuma au aluminiamu. Katika hali hii ya kushikilliwa
na chuma au aluminiamu inafnya kirutubisho hiki (P) kisiweza kuyeyuka katika
maji yaliyoko katika udongo na kuweza kuchukuliwa na mmea. Tatizo hili ni
kubwa sana katika nchi za joto zenye udongo uliokuwa na madini ya chuma kwa
wingi. Hii ni mojawapo ya sababu zinazofanya kuwepo na upungufu wa
fosiforasi inayohitajika kuchukuliwa na mmea ingawaje kirutubisho hiki kipo kwa
wingi katika aina nyingi za udongo (lakini katika hali ambayo haiwezai
kuchukuliwa na mimea).
Katika udongo wenye tindikali ya kiwango zaidi ya 7 (hujulikana kama udongo
wenye chumvichumvi), fosiforasi hushikiliwa na madini ya chokaa na katika hali
hii mmea hauwezai kuchukua hiyo fosiforasi iliyoshikamana na chokaa. Kwa
hiyo fosiforasi huweza kupatikana katika hali ambayo inaweza kuchukuliwa na
mmea kama tindikali ya udongo itakuwa kati ya 5.5 - 7.5. Mfano wa udongo huu
unapatikana karibu na Tororo Mashariki mwa Uganda.
4
Foriforasi katika Udongo

Page 5
Kwa asili katika udongo kuna madini yenye fosiforasi. Madini haya
yanapoyeyuka huingia polepole katika maji yalipo kwenye udongo. Mboji iliyoko
kwenye udongo pia ina fosiforasi. Viumbe vidogo vilivyoko katika udongo
huozesha mboji na kuifanya fosiforasi iwe katika hali ambayo itayeyuka katika
maji (H2P0-
4) na kunyonywa na mizizi ya mimea.
Fosiforasi katika udongo inavyonyonywa na mizizi ya mmiea.
Tatizo hili la fosiforasi kushikiliwa na madini ya chuma, aluminiamu na chokaa
katika udogo, wakilima wengi wanahitajika kuongeza virutubisho hivi kwa
kutumia aina mbalimbali za mbolea zenye virutubisho vya fosiforasi. Mojawapo
ya mbolea zenye kirutubishao hiki ni:
Mbolea za viwandani kama SSP, TSP, DAP.
Miamba ya Fosiforasi kama ile inayochimbwa kule Minjingu, Tanzania
("Minjingu Phosphate Rock)
Mbolea aina ya samadi, mabaki ya mazao shambani, majni yanayofukiwa
mabichi kama mikunde na mboji.
5
Ni jinsi gani fosiforasi huchukuliwa na mimea?

Page 6
Mimea hupata virutubisho muhimu kwa ajili ya ukuaji katika udongo. Mizizi ya
mimea hunyonya maji yalioko kwenye udongo yakiwa na virutubisho hivi. Na
ndio maana fosiforasi huchukuliwa na mimea ikiwa tu iko katika hali ya kuyeyuka
katika maji yalioko kwenye udongo.
Kama ilivyo Naitrojeni, fosiforasi pia ni muhimu kwa ukuaji na ustawi wa mazao.
Hufanya kazi zifuatazo katika mimea:
Husaidia ukuaji wa mizizi.
Huharakisha kukomaa kwa mazao (kuchanua, uzaaji wa matunda na mbegu)
Huimarisha ubora wa mazao (hasa mazao ya mboga mboga).
Fosiforasi pia ni muhimu sana katika utengenezaji wa nitrogeni iliyoko hewani
kuwa katika hali ambayo inaweza kutumiwa na mimea hasa ile ya aina ya
mikunde.
Kiasi cha P kinachotakiwa kwa ukuaji mzuri wa mimea kinategemea aina na umri
wa mmea. Upungufu wa virutubisho vya fosiforasi hutokea wakati mimea
inapokuwa midogo au miche wakati mizizi bado midogo. Mmea mdogo
unapokuwa haupati fosiforasi ya kutosha, uwezo wake wa kukua utakuwa
umeathiriwa. Kwa hiyo ukuaji mzuri wa mizizi ni muhimu sana ili kuwa na
mwanzo mzuri wa ukuaji wa mmea. Mmea mdogo unahitaji P kwa wingi wakati
unapoanza kukua, kiasi kingine unapoendelea kukua na kiasi kingine kitasaidia
wakati wa kuzaa matunda na mbegu.
Kuna aina ya mazao ambayo huhitaji fosiforasi kwa wingi. Baadhi yake ni:-
- Mahindi
- Kabichi
- Viazi
- Maharage, na aina nyingine za mikunde
- Aina nyingi za mboga.
Mimea mingine ina uwezo mkubwa wa kutafuta na kuchukua fosiforasi katika
udongo. Mimea hii ni kama:-
- Sukuma Wiki
- Mbaazi
- Alizeti mwitu.
6
Ni namna gani udongo hupungukiwa virutubisho vya
fosiforasi?

Page 7
Kuna mambo mawili muhimu yanaosababisha udongo wa nchi za kusini mwa
jangwa la Sahara, barani Africa kuwa na upungufu wa virutubisho vya fosiforasi.
1. Mchakato wa asili
Ukilinganisha na udongo wa nchi kama Amerika Kaskazini, Ulaya na Asia, aina
nyingi za udongo ulioko kusini mwa Jangwa la Sahara barani Afrika unarutuba
ndogo. Kwa muda mrefu virutubisho hivi vimepotea kutokana na mvua nyingi
(hufanya viende chini zaidi na mmomonyoko wa udongo), joto kali na michakato
ya kikemia ambayo hutokea katika miamba. Matokeo yake, udongo wa kichanga
na udongo unaotokana na miamba ya granites, ndiyo uliopo kwa wingi. Udongo
huu una virutubisho haba na uwezo mdogo wa kuhifadhi maji.
2. Kazi za binadamu
Upungufu wa fosiforasi katika udongo pia husababishwa na kazi za wanadamu
na jinsi wanavyohudumia mashamba yao. Kulima mazao mengi kwa mfululizo
na kuvuna huondoa fosiforasi kwenye udongo. Uhudumiaji mbaya wa
mashamba kama vile kuchoma mabaki ya mazao shambani, kutoongeza mboji
katika udongo na kulima kunakosababisha mmomonyoko wa udongo
vimechangia sana kupungua kwa fosiforasi katika udongo. Kazi/shuhguli zote
hizi zimefanya udongo katika mashamba ya wakulima uchoke.
7
Source: IIRR, 1998
Ni namna gani udongo hupungukiwa virutubisho vya
fosiforasi?

Page 8
Mzunguuko wa fosiforasi
Mchoro huu (hapa chini) unaonyesha mzunguuko wa fosiforasi na unaonyesha
namna fosiforasi inavyoweza kuongezwa na kutolewa katika mfumo wa udongo.
Viwango vya virutubisho katika mfumo wa udongo
Viwango vya virutubisho katika udongo vinaweza kufananishwa na maji katika
pipa au tanki la kutunzia maji ambapo familia nyingi wanayo katika maeneo
wanayoishi. Fikiria kwamba kinamama wameenda kuchota maji katika vyanzo
vya maji au visima vilivyopo karibu na kaya zao na hatimaye wakaweza kujaza
hilo pipa. Baada ya siku chache maji haya yalitumika kufulia nguo, kupikia,
kuogea na pia kunywa. Kwa kuendelea kutumia maji hayo, itafikia wakati
yatakuwa yamekwisha. Kama mtu ataamua kuchota tena na kujaza lile tanki,
maji yatakuwepo kwa ajili ya matumizi ya familia. Lakini kama maji hayatachotwa
pindi yanapokuwa yamepungua, itafikia wakati kutakuwa hakuna maji kwa ajili ya
matumizi ya nyumbani. Maji ni muhimu, bila maji huwezi kupika chakula, kufua,
n.k.
8

Page 9
Kina mama wanachota maji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.
Kuongeza P katika udongo pia ni muhimu kama chakula cha
mimea ambacho hupungua kila mazao yanapovunwa
Picha imechorwa na Petra Rohr-Roundaar
Kumbuka: Mfano wa kuongeza maji kila yanapoisha kwenye pipa unaweza kusaidia wakati
unapowaeleza wakulima kuhusu umuhimu wa kuongeza P kwenye udongo.
Kwa sasa kuna tatizo kubwa la rutuba ya udongo kwa sababu wakulima
wanapanda na kuvuna tu mazao bila kurudishia virutubisho vilivyochukuliwa na
mimea kama chakula wakati ilipokuwa shambani. Hali hii ya kutokuwepo na
uwiano wa kutoa na kurudishia virutubisho katika udongo, imesababisha
uzalishaji mdogo na uhaba wa chakula katika maeneo mengi ya Bara la Afrika
9
Virutibisho vilivyoko katika udongo ni
muhimu kwa ukuaji wa mazao, kama
ilivyo maji kwa kila kaya. Maji unaweza
kupata kupitia mvua. Lakini huwezi kupata
P kutoka hewani. Wakulima wanapovuna
mazao, wanakuwa pia wameondoa P
ambayo ilichukuliwa au kunyonywa na
mimea hiyo kama chakula wakati
ilipokuwa shambani. Kama mfano wa maji
uliolezwa hapo juu, kwamba maji lazima
yaongezwe kila yanapokuwa yameisha
kwenye pipa, ndiyvo hivyo P
inavyopungua wakati mazao
yanapovunwa shambani na kiasi hiki
kilichopungua kinahitajika kirudishiwe kwa
ajili ya kutumiwa na mazao mengine
yatakayopandwa.

Page 10
Wakati ardhi inapotumika kwa kilimo, virutibisho
vinapotea katika udongo kwa njia nyingi. Kuvuna
mazao, mfano kama mahindi na mboga-mboga
yanapovunwa yanachukua kiasi kikubwa cha
virutubisho katika udongo. Pamoja na hili,
virutubisho vya mimea pia vinapotea kupitia maji
yanapoenda sana chini pamoja na mmomonyoko
wa udongo. Kwa hivyo ili kufanya kuwepo na
uwiano katika ya virutibisho vinavyochukuliwa na
mimea na vile vinavyorudhishiwa, kuna umuhimu
wa kuongezea viwango hivyo katika udongo ili
kufidia vile vinavyopotea.
Virutubisho vingi vinachukuliwa kutoka kwenye udongo kuliko vile vinavyorudishwa. Hii inafanya
kutokuwepo na uwiano wa virutubisho na inaathiri sana uzalishaji kwa wakulima wadogowadogo
katika Afrika.
Wakulima wana ufahamu wa karibu kuhusu mashamba na mazao yao. Ni
wachunguzi wazuri na mara nyingi hutambua hali ya udongo au ardhi kuchoka.
Wakulima wanaweza kushindwa kuonesha tatizo na kusema hasa kwamba
linasababishwa na nini, lakini wanaweza kutambua maeneo au hali
zinazohusiana na tatizo hilo.
Kufanya kazi kushirikiana na wakulima kuchunguza kama mazao yao
yanaathirika na upungufu wa fosifarasi katika udongo inasaidia. Kama Afisa
Ugani ataweza kujenga uwezo wa wakulima kutambua matatizo ya ukosefu wa
fosforasi wao wenyewe, wakulima wataona umuhimu wa P katika kuzalisha
mazao mazuri. Akiwa na ufahamu zaidi wa aina za pembejeo zinzoongeza P
katika udongo, mkulima ataweza kujitegemea zaidi na kuchukua hatua
kuhusiana na upungufu wa virutubisho katika udongo.
Kuna mbinu na majaribio mbalimbali zinazoweza kutumika kutathmini rutuba ya
udongo na upungufu wa virutubisho. Kupima udongo na mimea kunaweza
kufanyika kujua kiwango/kiasi cha rutuba au virutubisho katika udongo, lakini njia
hii inahitaji mtu aliyesomea upimaji huu ambaye atapima katka maabara na
kusoma matokeo.
Mbinu nyingine inayoweza kutumika kuchunguza viwango vya virutubisho katika
udongo ni kuangalia kwa macho. Wakati mmea unapokosa virutubisho
unavyohitaji kwa kukua vizuri, huonyesha dalili maalumu. Dalili hizi zinaweza
kutumika kugundua upungufu wa virutubisho. Uchunguzi kwa kutumia macho
hauchukui muda mrefu sana na hauhitaji chombo maalumu au chombo cha
maabara.
10
Kutambua upungufu wa Fosiforasi katika udongo

Page 11
Wakulima wanaweza kuelekezwa kufanya utambuzi wa kuona ukosefu wa
madini ya fosiforasi kama ifuatayo ni
Kutana na vikundi vya wakulima na tumia muda wa kutosha kuwaelezea
wakulima umuhimu wa madini ya fosforasi kwa mimea kutokana na maelekezo
uliyoyasoma katika toleo hili. Tumia picha kubwa za mabango na maelezo
yaliyomo katika toleo hili ili kuelezea umuhimu wa madini ya fosiforasi. Waulize
wakulima kuhusu pembejeo mbalimbali wanazotumia kuongeza virutubisho
katika mashamba yao. Tembea pamoja na wakulima ili kuona kwa macho
kugundua upungufu wa fosforasi kwenye zao la mahindi. Amueni kama kikundi
kupita njia itakayowapitisha katika sehemu zenye sura tofauti za nchi - milima na
mabonde. Tembeleeni mashamba yaliyohudumiwa kwa mbinu mbalimbali. Kwa
ujumla mahindi ni kati ya mimea katika kuonesha upungufu wa fosforasi. Kwa
hiyo ni muhimu kufanya zoezi hili wakati wa msimu wakati mahindi
yameshakuwa na majani. Chukua daftari na kalamu (penseli) na kusanya
sampuli za majani kadiri mnavyotembea ili mlinganishe kutoka shamba moja na
lingine. Ikiwezekana, chukua kipima tindikali kupima udongo kama una tindikali
au nyongo.
11
Kutumia njia shirikishi katika kuchunguza kwa kutazama

Page 12
kutoka: IIRR, 1998
Hatua za msingi katika zoezi la kugundua kwa kuona shambani
1. Kutambua kwamba kuna matatizo shambani.
Waulize wakulima kutaja kama wanaona dalili za kasoro zozote katika
kila shamba husika au iashiria kwamba mimea haikuwi kama
inavyotakiwa katika hali ya kawaida.
2. Yanayojitokeza yasiyo ya kawaida.
Pamoja tuchunguze mimea na tupate kujua
yasiyo ya kawaida kutokana na rangi na muundo wa udongo.
3. Usababishaji.
12

Page 13
Uliza wakulima maswali ili
waweze kujua chanzo cha
shida yenyewe. Chunguza
mimea lakini pia hakikisha
utumiaji bora wa shamba.
Maswali ya kujadili:
Je kuna tatizo la maji? Mvua ni
nyingi sana, au mvua ni kidogo
sana?
Je kuna tatizo la wanyama au
wadudu waharibifu wa mazao?
Je mbegu iliyopandwa ni ya
kisasa, chotara, au ya kienyeji?
Je ni sehemu gani katika shamba
ambapo matatizo yamejitokeza?
Je ni aina gani ya ulimaji imetumika kwa upandaji? Je njia hii ni tofauti na ile
ambayo wakulima hutumia?
Je ni kipi kilichobadilika (mavuno au ubora wa ardhi)?
Je hali ikoje ukilinganisha na msimu uliopita? Hali ikoje ukilinganisha na
shamba la jirani?
Endapo udhaifu upo kwenye majani je hali mbaya sana ipo katika majani
machanga au majani yaliyokomaa?
Je ni tatizo la mmea kutokuwa na rangi ni kwenye michirizi ya majani (veins)
na pembeni mwa jani au kwenye jani lote?
Je jani limekauka na kufa?
Je kuna kuna hali isiyoyakawaida katika maua na matunda?
4. Kutoa maelezo yasiyo na msingi
Linganisha sehemu zilizo nzuri na zile zilizo mbaya katika mmea mmoja na
kujadili au kutafakari tofauti zilizopo
Jaribu kufafanua au kurahisisha mambo ya msingi yatokanayo na ugunduzi
uliokwisha fanywa
Kama tatizo ni upungufu wa virutubisho katika mojawapo ya mimea ndani ya
shamba ni wazi kwamba mimea yote katika eneo hilo itakuwa imeathirika. Katika
kila mmea majani yote yaliyo na umri mmoja yataonyesha dalili zinazofanana.
Kama kuna tofauti zinazo jionyesha basi zinaweza kuwa ni tofauti za eneo moja
na jingine, aina ya udongo au aina ya kilimo kitumikacho.
Hiki ni kielelezo cha jani la mahindi lililo na afya na nguvu.
13
Imechorwa na Njoroge

Page 14
Wakulima wakiona rangi yenye mwelekeo wa njano katika majani ya mahindi
(kama ilivyo katika picha hapa chini) ambapo badiliko la rangi huanzia kwenye
ncha na kuendelea katikati ya jani kuelekea kwenye mshipa wa kati, hii ni dalili
ya ukosefu wa Naitrogeni (N).
Wakulima wakiona rangi yenye mwelekeo wa njano katika majani ya mahindi
(kama ilivyo katika picha hapa chini) ambapo badiliko la rangi huanzia kwenye
sehemu ya nje ya jani la mahindi hii ni dalili ya ukosefu wa madini ya Potasium
(P).
Kama tatizo ni upungufu wa madini ya fosiforasi dalili zifuatazo zitajionyesha
katika mmea:
➢ mmea kudumaa
➢ mmea kuwa na rangi ya bluu kijani nzito au rangi ya zambarao kwenye
majani yaliyokomaa (tazama kielelezo cha jani mahindi chini)
➢ Mizizi haikui
➢ Kuchelewa kukomaa, mbegu dhaifu na udhaifu katika kutengeneza matunda
14

Page 15
Kugundua kwa Kutazama - Faida na Madhara
Kugundua kwa Kutazama - Faida na Madhara
Njia ya kutazama au kuona kama ilivyoelezewa hapo juu, ni njia ya haraka na
nyepesi kugundua kama mimea ina matatizo ya ukosefu wa virutubisho bila
kutegemea huduma au ushauri wa afisa kilimo au fundi wa maabara. Mara tu
upungufu unapogunduliwa, mkulima anaweza kuweka mikakati
itakayomuwezesha yeye kurekebisha tatizo (ikiwemo kuongeza mboji).
Njia ya kuona au kutazama ina madhara kadhaa: Ni lazima tatizo lijionyeshe
kwanza ndipo liweze kugunduliwa na kwa hali hiyo mmea utakuwa umekwisha
athirika na hasa mimea ile ya msimu mfano mahindi na si rahisi kurekebisha
tatizo hilo hasa kwa mmea huo.
Kuona au kutazama ni mchakato unaofanana sana na vile daktari anavyoweza
kugundua ugonjwa hasa kwa kumtazama mgonjwa. Ingawa njia hii inaweza
kuwa ya msaada, hasa kwa daktari ambaye ana uzoefu wa kutosha bado si njia
ya kisayansi. Hata daktari aliye mahiri atapenda kuwa makini na ugonjwa
wenyewe kwa kuichunguza damu au kuchukua picha ya x-ray kutokana na tatizo
lenyewe.
15
A.Ukosefu wa naitrogeni B. Ukosefu wa madini ya potasium C. Ukosefu wa fosiforasi

Page 16
Kwa wakulima walio wengi 'kuona ni kuamini'. Njia nzuri ya kugundua kama
fosforasi ni tatizo katika ukuaji wa mimea ni kufanya majaribio katika mashamba
ya wakulima walio tayari na mashamba yao yatakuwa ya mfano. Majaribio
yanaweza kupangwa na vikundi vya wakulima wakishirikiana na Bwanashamba
16
Majaribio shambani
chanzo :IIRR, 1998

Page 17
na wao wenyewe wanaweza kuamua aina ya kilimo au aina ya mazao
watakayopenda kupanda kwenye majaribio yao. Wanaweza kuchagua kupanda
mahindi au mazao mengine kama jamii ya maharage. Sehemu moja isiwekwe
mbolea yoyote na maeneo mengine yanaweza kuwekwa mboji, mbolea za
mimea iliyooza na mbole zinazoatoka mazizini. Wakulima wanaweza vilevile
kuweka mbolea za viwandani ambazo zina mchanganyiko wa fosforasi mfano
mbolea ya triple super phosphate (TSP) au rock phosphate (PR) ili kuona tofauti
kati ya mbolea za viwandani na mbole za asili kama chanzo cha fosforasi katika
ukuzaji wa mimea.
Hakuna sheria maalum za kufuata, jambo la msingi ni kuongeza mazoezi au
uzoefu wa majaribio kwa wakulima na kuimarisha uelewa wao kuhusu umuhimu
wa fosforasi kwa mimea. Zoezi hili pia hujenga uwezo wa wakulima (ujuzi, kuwa
katika vikundi na kushirikiana) katika kuanzisha majaribio yao wenyewe. Hatua
muhimu za kufuta wakati wa kuanzisha jaribio ni kama ifuatavyo:
➢ Kuangalia uzoefu wa wakulima kwa vipindi vya nyuma (ni majaribio gani
walikwisha fanya kabla? Walifanyaje? Kwanini walifanya hivyo, je
walifanikiwa?
➢ Kubuni na kupanga majaribio na wakulima (ni wakina nani hasa watahusika
na kufanya majaribio? Je kuwepo na majaribio ya kuweza kutumika kama
vielelezo (controls)? Je ni maeneo yapi yatakuwa muafaka kwa majariobio?
Ni maeneo kiasi gani yanahitajika? Ni vitu gani vinahitajika kutumika? Jaribio
litapangwa vipi? Ni vitu gani vinahitajika na vitapatikanaje?
➢ Kuweka utaratibu wa kutathmini majaribio (ni vigezo gani vitumike katika
kutathmini yaliyotokea kwenye majaribio? Nini na ni lini itahitajika kuangalia,
kupima kujadili na kuweka kumbukumbu na haya yote yatafanyikaje? Ni nani
atahusika?
➢ Wakulima watangaziwe. Pengine wengine watapenda kushirikiana na
wakulima wengine katika kupima mafanikio yao. Mafunzo ya mkulima kwa
mkulima ni nafasi au muda muafaka kwa ajili ya kuwashirikisha wakulima
kwenye majadiliano na kubadilishana uzoefu. Kuwaalika wakulima toka
makundi mengine kutembelea mashamba ya majaribio ni jambo lingine katika
kubadilishana matokeo ya majaribio na kuwafundisha wengine umuhimu wa
fosiforasi kwa ukuaji wa mazao.
Muhimu ni vikundi vya wakulima kukutana mara kwa mara katika maeneo
ambapo majaribio yapo kwa kufuatilia na kutathmini majaribio.
Kutoka kwa Bashir Jama, muunganishaji wa Afrika mashariki na kati katika
ICRAF,
kuhusu maonyesho katika mashamba.
Magharibi mwa Kenya, mna ploti ndogo ndogo zinazotumika kudhbitisha
upungufu wa madini. Hizo ploti huwa 3x3m na huwa na:
17

Page 18
1) Hamna chochote
2) Nitrogeni pekee
3) fosiforasi pekee
4) Nitrogeni na Fosiforasi pamoja
Kiwango cha Nitrogeni na Fosiforasi huwa juu, kama kilo mia moja kwa ekari.
Waweza kuwa na ploti kama hizo 2-3 katika sehemu mbalimbali katika
shamba au mashamba na zisetiwe na afisa wa ektensheni na/au wakulima
walioelimika. Mmea wa majaribio ni mahindi. Matokeo ya kutumia fosiforasi
kwa udongo unaoshukiwa kukosa fosiforasi huwa ni ya umuhimu kwa elimu
ya wakulima na maafisa wa ekstensheni.
Kama katika kuona, kutazama au kufanya majaribio shambani upungufu wa
fosiforasi ulionekana, ni kwa jinsi gani mkulima anaweza kushughulikia tatizo
hili? Kumbuka kwamba vyanzo vyote vya fosforasi vikiwa vya viwandani au asili
ni muhimu kwa afya ya mmea. Zifuatazo ni pembejeo mbalimbali ambazo
mkulima anaweza kuweka kwenye udongo ili kuongeza kiasi cha fosiforasi ili
kulisha na kuongeza mazao.
Mbolea zinazotokana na kuoza kwa
Majani mabichi ya mikunde
Mboji
Mwamba wa fosiforasi
Mbolea ya fosiforasi iliyotengenezwa kiwandani
Kinyesi cha wanyama - samadi
Masalia ya mimea iliyokatwa na kuachwa ioze
Mbolea ya viwandani na ile ya miamba
Mwamba wa fosiforasi
Mbolea ya fosiforasi iliyotengenezwa kiwandani
Mbolea hizi zote zina faida na matatizo yanayohusiana nazo. Kwa mfano mbolea
ya samadi inaweza kuongeza virutubisho muhimu katika udongo lakini vilevile
inaweza kuongeza kiasi cha tindikali ardhini. Unaweza kurejea mjadala wetu wa
awali kwamba udongo wenye tindikali unasababisha kukamatwa kwa kirutubisho
cha fosiforasi na hivyo kusababisha kirutubisho hiki kutopatikana kwa matumizi
ya mmea au mazao.
18
Vyanzo vya fosiforasi vinavyoweza kuboresha rutuba ya
udongo

Page 19
Kwenye sura hii, tumejadili kuhusu chokaa kama kirutubisho muhimu kwa ajili ya
ukuaji na afya ya mimea. Usome kuhusu jinsi chokaa inavyokuwa kwenye
udongo, na usome kuhusu mambo yanayojitokeza endapo chokaa ipo au
inapokuwa imezuiwa na viasili vingine. Pia umejifunza jinsi chokaa inavyoweza
kumalizwa ardhini. Maelezo kuhusu kugundua uwepo au kutokuwepo kwa
chokaa kwa njia ya kuona na kwa njia ya kufanya majaribio yamewezeshwa
kwako ili kukupa uelewa wa kuweza kufanya kazi na wakulima ili kuweza
kugundua upungufu wa chokaa katika mashamba yao. Mwisho, tumekutajia
vyanzo mbalimbali vya chokaa katika mbolea za viwandani na zile za kiasili
ambazo zinaweza kutumiwa kuongeza kiasi cha chokaa pindi zinapowekwa
kwenye udongo kwa ajili ya matumizi ya mimea.
Maneno ya kiutalaamu na maana zake
Udongo wenye chachu Udongo wenye kiwango cha pH ya chini ya 7.0.
Udongo wenye chumvichumvi udongo wenye pH zaidi ya 7.0
Mboji Mbolea iliyotokana na kuoza kwa mabaki ya mimea.
Zao Zao la msimu au la muda mrefu shambani ambayo hulimwa nakutumiwa
na wanadamu.
Mmomonyoko wa udongo Udongo kuchukuliwa na maji au upepo
Mbolea huwekwa katika udongo kwa lengo la kuongeza virutubisho katika
udongo kwa ajili ya ukuaji wa mimea
Mbolea ya kijani majani mabichi huwekwa katika udongo kwa lengo la
kurutubisha udongo.
Pembejeo Vitu ambavyo mkulima hutumia katika mfumo mzima wa kilimo kwa
lengo la kuboresha uzalishaji mfano mbolea, maji, mbegu, madawa n.k.
Fosiforasi kushikiliwa katika udongo Mchakato unaofanya fosiforasi isiweze
kuchukuliwa na mimea katika udongo
Rutuba ya udongo Ubora wa udongo kuweza kutoa virutubisho kuchukuliwa
na mimea katika kiwango kile kinachohitajika na mmea na kuwezesha kukua
vizuri
19
Kwakifupi

Page 20
pH ya Udongo Kiwango cha uchachu au chumvichumvi iliyoko katika udongo.
Viwango hivi huanzia 0 mpaka 14 na 7 ndio kiwango cha kati ambacho udongo
unakuwa hauna chachu wala chumvichumvi.
Myeyuko Uwezo wa kuweza kuyeyuka katika maji (mfano sukari huweza
kuyeyuka katika chai).
20